Tuesday, 1 April 2014

FA YAJA NA MBINU MPYA KUELEKEA BRAZIL MWAKA HUU



Huenda dunia ikashanga haswa kwa wale mashabiki wa timu ya taifa ya Brazil pale watakapo shuhudia timu ya taifa ya uingereza ikivaa jezi sawa na zile za kwao katika moja ya mechi za kombe la dunia mwaka huu huko Brazil.

Chama cha soka cha Uingereza FA kimetoa aina ya jezi amabazo timu hiyo itatumia kwenye fainali hizo za kombe la dunia mwezi wa sita mwaka huu, zikiwa na rangi nyeupe lakini pia za ugenini zikiwa na rangi nyekundu huku zikiwa chini ya wadhamini wao wakubwa Nike.
RANGI NYEUPE AMBALO NI CHAGUO LA KWANZA
RANGI NYEKUNDU AMBALO NI CHAGUO LA PILI

Lakini habari za ndani ya FA zinasema kuwa kwa kushirikiana na wadhamini wao Nike wanajiandaa kutoa jezi za rangi ya njano ambazo zitakuwa sawa kabisa na zili za wandaaji wa fainali hizo za kombe la dunia yani Brazil.

HII NDO JEZI AMBAYO ITAFANANA NA ZILE ZA BRAZIL
Moja ya kiongozi wa FA alisikika akisema kuwa kama wanataka kucheza kama Brazil basi lazima wajiandae kuwa kama Brazil kuanzia kimavazi ili kufikia kiwango cha timu hiyo, lakini amebainisha kuwa huenda jezi hizo zikatumika kwenye fainali kama watafanikiwa kufika hatua hiyo kubwa kabisa.

Kwa mujibu wa wa taarifa ya ndani kwenye chama hiko ni kuwa jezi hizo ambazo zitatumiwa na timu hiyo huko Brazilb zitakuwa sokoni kuanzia jumatatu, na mashabiki wa timu hiyo wanazisubiri kwa hamu sana kutokana na jinsi zilivyo.

No comments:

Post a Comment