Wednesday, 16 April 2014

GARETH BALE ASIBITISHA KUWA YEYE NIA HATARI BAADA YA KUIPATIA REAL UBINGWA WA 19 WA COPA DEL REY



Real Madrid katika picha ya ubingwa


Real  Madrid wameweza kuibuka na ushindi wa magoli  mawili kwa kwa moja dhidi ya mahasimu wao wakubwa Barcelona katika mchezo wa fainali wa kombe la Copa del rey.

Real wao ndio walikuwa wa kwanza kupachika goli kunako dk ya 11 kupitia kwa Angel Di maria,  na hivyo kufanya hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Real walitoka wakiwa kifua mbele katika awamu hiyo.

Kunako kipindi cha pili  katika dk ya 68 kinda wa Barcelona  Marco  Bartra aliweza kusawazisha bao hilo kupitia mpira wa kichwa baada ya kuitumia vizuri kona iliyo chongwa na nahoza wake Xavi.

Baada ya goli hilo Barcelona waliweza kuamka na kujaribu kuonyesha mpira ulio takata  kama ilivyo kawaida yao, lakini kunako dakika za lala salama Gareth Bale aliweza kuifungia real goli la ushindi.
di maria akishanglia goli la kwanza

Bale aliweza kusibitisha kuwa yeye ni mchezaji ghali zaidi duniani baada ya kumshinda mbio kinda Marco Bartra na kwenda kumuona golikipa Pito kunako dk ya 85 ya mchezo huo.

bale akishangilia goli la ushindi
Mchezo huo ambao ulitawaliwa na kadi 5 za njano pia ulikuwa ni mchezo usio isha tamwe za hapa na pale baina ya wachezaji wa timu hizi mbili, huku real wakiwa wameshuka dimbani bila ya Cristian Ronaldo baada ya kupata majeraha ya nyama za pacha katika mechi iliyopita.

Hii inakuwa ni kwa mara ya 19 kwa real madrid walio chini ya Carlo Ancelotti kuweza kuchukuwa kombe hili la Copa Del Rey  tangu lianzishwe na mara ya mwisho walichukuwa mwa 2010-2011 na mara ya kwanza ilikuwa ni 1905.

hakuna kama mimi
Hili linakuwa ni kombe la kwnza kwa Real Madrid kuweza kuchukuwa katika msimu huu, huku wakiwa bado katika kugombania ubingwa wa ligi dhidi ya vinara wa ligi hiyo kwa sasa ambao ni Atiletico De Madrid wenye alma 82 kwa 79 za real.

Lakini pia unakuwa ni ubingwa wa kwanza kwa Carlo Ancelotti akiwa na klabu hiyo huku bado akiwa na kibarua kizito cha kuipatia Real ubingwa wa mara ya 10 wa klabu bingwa barani ulaya baada ya kuingia hatua ya nusu fainali na watakipiga na Bayern Munich ya Ujerumani tarehe 22 mwezi huu.

No comments:

Post a Comment