

Baada ya mchezo wa mwishoni mwa wiki dhidi ya JKT Ruvu, kikosi cha Young Africans jana jioni kiliingia kambini mjini Bagamoyo na kufanya mazoezi jana na leo asubuhi kwenye Uwanja wa Boko Beach Veteran eneo la Boko.
Kuelekea mchezo huo wa kesho Kocha Mkuu Hans amesema vijana wake 20 walioingia kambini wote wapo kwenye hali nzuri, kiafya, kifikra na morali ya kusaka pointi 3 ni ya hali ya juu kwani vijana wanahitaji kutetea Ubingwa tena kwa msimu wa pili mfululizo.
Katika mchezo wa awali uliozikutanisha Kagera Sugar na Young Africans katika uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Young Africans iliweza kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 wafungaji wakiwa ni Mrisho Ngasa na Hamisi Kizza.
Wachezaji Haruna Niyonzima, David Luhende, Athuman Idd, Emmanuel Okwi waliokuwa wagonjwa wanaendelea vizuri na watarajiwa kuungana na wenzao mara baada ya mchezo dhidi ya JKT Ruvu pamoja na mlinzi Kelvin Yondani aliyekua na kadi 3 za njano.
No comments:
Post a Comment