Tuesday, 1 April 2014

USIKU WA UEFA: MOYES KUUKWAA MSITU WA PEP GUADIOLA

Michuano ya hatua ya robo fainali ya klabu bingwa barani ulaya inaendelea hii leo kwa kuzikutanisha timu kubwa nne kutoka ligi kuu tatu tofauti barani ulaya ambazo ni Ujerumani, Uingereza, Spain, huku tukishuhu timu tatu kati ya timu nane zilizoingia kwenye hatua ya robo fainali zikitoka kati la liga.

Mashetani wekundu ambao wamekuwa na matokeo mabaya kwa msimu huu leo hii watawakaribisha mabigwa watetezi wa taji hilo na mabingwa wapya wa ligi kuu ya Ujerumani  Bayern Munich katika dimba la Old Traford.

Kocha David Moyes anategemea kukutana na upinzani mkubwa kutoka kwa mabingwa hao wa ujerumani kutokana na kikosi walichonacho msimu huu ambacho kimeweka rekodi ya kuchukuwa ubingwa huku wakiwa na mechi saba mkononi ikiwa ni chini ya Pep Guadiola.

Laini kwa upande wa mechi nyingine hii leo Barcelona itaikaribisha Atletico Madrid, ambao wote wanatoka kwenye ligi moja ya la liga huku wakichuana vikali kunyakuwa taji la ligi hiyo huku nafasi kubwa ya kunyakuwa taji hilo akipewa Atletico de Madrid

No comments:

Post a Comment