Thursday, 3 April 2014

CHELSEA YALALA PARIS..

Paris Saint-Germain, wakicheza Uwanja wa kwao Parc des Princes huko Paris, France, Usiku huu wameichapa Chelsea Bao 3-1 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE

Ezequiel Lavezzi alitangulia kuwapa PSG Bao la kuongoza katika Dakika ya 4 baada kuweka gambani Mpira uliookolewa kwa Kichwa na John Terry na kufumua Shuti moja kwa moja na kumpita Kipa Petr Cech.

lavezzi akishangilia goli
Chelsea walisawazisha kwa Penati ya Dakika ya 27 iliyopigwa na Eden Hazard na ilitolewa na Refa Milorad Mazic kutoka Serbia alipoamua Sentahafu wa PSG Thiago Silva ‘kamwangusha’ Oscar.
Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 1-1.

PSG walifunga Bao lao la 2 baada ya Ezequiel Lavezzi kupiga mpira safi ambayo Kipa Petr Cech alishindwa kuzuia na kumparaza Zlatan Ibrahimovic kisha Mchezaji wa Chelsea David Luiz kuusindikiza wavuni.

Ibra kadabra akiwa kwenye maumivu makali ya misuli
Mchezaji alietoka Benchi, Javier Pastore, aliipa PSG Bao la 3 katika Dakika ya 90 baada ya kupokea Mpira wa kurushwa na kuwatoka Cesar Azpilicueta, Frank Lampard na John Terry kisha kupiga Shuti la chini chini na kumshinda Kipa Petr Cech,
timu hizi zitarudiana huko Stamford Bridge Jumanne Aprili 8.


1 comment:

  1. sikutegemea kama hawa PSG wanaweza ichalaza Chelsea

    ReplyDelete