Wednesday, 2 April 2014

MADRID YALIPA KISASI CHA MWAKA JANA HUKU RONALDO AKIWEKA REKODI YA GOLI 14 KATIKA MECHI 8 ZA UEFA MSIMU HUU

Real Madrid, wakicheza Uwanjan kwao Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain, wameichapa Borussia Dortmund Bao 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE.

Gareth Bale ndie aliefunga Bao la Kwanza katika Dakika ya 3 tu baada kuunganisha pasi safi ya Daniel Carvajal na kumzidi akili Kipa Roman Weidenfeller

bale akiwa kazini
Bao la Pili la Real lilifungwa katika Dakika ya 27 kupitia Isco kwa Shuti la chini toka Mita 20.
Hadi Mapumziko  ilikuwa Real 2 Dortmund 0.

Katika Dakika ya 57, Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, alipiga Bao la 3 baada kumtoka Kipa Roman Weidenfeller kufuatia kupokea pasi safi ya Luka Modric.

Likiwa ni bao la 14 kwa Ronaldo kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu huu na ameifikia Rekodi  ya Lionel Messi aliyefunga Bao 14 katika Mechi 11 za UEFA CHAMPIONS LEAGUE msimu wa 2011/12 wakati Ronaldo amechukua Mechi 8 tu. 

bale na ronaldo wakipongezana
Lakini laweza kuwa pigo au laa maana Ronaldo hakumaliza Mechi hii baada ya kuumia na kutolewa nje katika Dakika ya 80 na hadi sasa bado haijajulikana kama atakuwa tayar akatika mechi ya marudiano huko
Signal Iduna Park, Jijini Dortmund, Germany Jumanne Aprili 8.

No comments:

Post a Comment