Tuesday, 8 April 2014

EMMANUEL ADEBAYOR NA WENZAKE WAIRUDISHA UNITED MTAA WA SABA WAKISHINDA TANO KWA MOJA DHIDI YA SUNDERLAND



Mechi ya kiporo iliyochezwa jana usiku kati Tottenham na sunderland iliweza kutosha kuirudisha Manchester united katika nfasi yake ya saba ambayo imekuwa nafasi ya kudumu kwa klabu hiyo katika msimu huu ambao umekuwa wa majanga kwao.

Shukurani za pekee ziende kwake Emannuel  Adebayor kwa kuweza kupigilia misumari miwili katika ushindi wa goli tano kwa moja katika mchezo uliopigwa kunako dimba la white hart line, na sunderland wao ndiyo walikuwa wa kwanza kupata goli kunako dk ya 17 kupitia kwa Cattermole.

Lakini baadaye Adebayor aliuwasha moto wa kifuu kunako dk ya 28 huku Kane akimpokea kijiti hiko kunako dk ya 59 kwa kufunga goli la pili lakini Eriksen naye alipigilia msumari wa tatu katika dk 78 na baadaye tena Yule Yule Adebayor alipeleka msiba wan ne kunako dk ya 86.

Kabla ya mpira kumalizika yani katika dakika za lala salama yani dk 90 Sigurdsson aliweza kuihakikishia sunderland kuwa swala la wao kushuka daraja lipo pale pale baada ya kupiga goli la tano katika mchezo huo.


Kwa ushindi huo wa spurs ulitosha kuipeleka katika nafasi ya sita ya msimamo wa ligi na kuishusha Manchester United hadi nafasi ya saba kwa tofauti ya pointi mbili, lakini pia ushindi huo uliendelea kuibakiza sunderland katika jinamizi la kushuka daraja wakiwa katika nafasi ya mwisho na pointi 25.

Kocha wa sunderland Gus Poyet  amedai kuwa itahitajika maajabu wao kuweza kusalia katika ushindani wa ligi kuu ya uingereza kwa msimu ujao baada ya kuwa na matokeo mabaya na sasa wanashika nafasi 20 huku wakiwa wamecheza mechi 31 tofauti ya mechi mbili na Fulham na Cardiff walio nafasi ya 18, 19.

Kwa upande wa pili kocha wa Totternham Tim Sherwood alikaririwa akisema kuwa ilikuwa ni mechi nzuri na alifurahishwa sana na kiwango cha timu yake kwa jana japo kuwa kuna tetesi huenda akaachia ngazi mwisho wa msimu huu na kibarua hiko kikamuangukia  Louis Van Gaa.

No comments:

Post a Comment