Thursday, 10 April 2014

MAN UTD, BARCELONA WAANGA UEFA, BAYERN ATLETICO DE MADRID WAINGIA NUSU FAINALI UEFA



Manchester united jana walifikia mwisho wa safari yao ya kuelekea kwenye hatua ya nusu fainali ya klabu bingwa barani ulaya baada ya kupokea kichapo cha goli tatu kwa moja kutoka kwa mabingwa watetezi wa taji hilo Bayern Munich.

Magoli katika mechi hiyo yalifungwa na Patrice Evra kwa upande wa Man Utd kunako dk ya 57 huku Mario Manduzuck akisawazisha kunako dk ya 59 dk mbili baada ya goli la Patrice Evra, huku Muller akipigilia msumari wa pili katika dk ya 68 na Robben kumaliza katika dk ya 76.

Evra akiwa ofisin kwake
Ulikuwa ni usiku mzuri snana kwa Pep Guadiola baada ya kuweza kuvitoa vilabu viwili vikubwa kutoka katika ligi ya uingereza na kufika hatua ya nusu fainali huku wakiwa na ndoto za kulitetea taji lao kwa mara ya pili, Bayern ilianzia kwa Arsenal kwa kuwatoa na imemalizia kwa mashetani hao wekundu wa jiji la Manchester.

Dante akiongoza jahazi la furaha baada ya ushindi
Nao fc Barcelona jana waliweza kuyaaga mashindano hayo ya Uefa kwa kukubali kichapo cha goli moja kwa bila kutoka kwa vinara wa ligi ya Spain ama la liga yani Atletico De Madrid kwa bao la mapema tu kutoka kwa Koke katika dk 5.

Koke akishangilia goli lake
Ilikuwa ni safari nzuri kwa kocha Diego Simione kwa usiku wa jana kuweza kuvuka hatua hiyo ya robo na kuingia nusu fainali kwa kuwasambaratisha vigogo hao kutoka La massia , ilikuwa ni mechi ya kukata na shoka kwani wote wanatoka kwenye ligi moja na huku wakiwa wamefuatana wakwanza na wa pili.

tumemaliza kazi
Kwa matokeo ya jana na juzi yameweza kutoa timu nne ambazo zitamenyana kwenye hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo, Spain wao wamefanikiwa kutoa timu mbili kuelekea hatua hiyo ya nusu fainali ambazo ni Real Madrid na Atiletico De Madrid.

Chelsea ndiotimu pekee iliyoweza kuvuka kwa timu za uingereza baada ya kuwatoa Psg na Bayern Munich imeweza kuiwakilisha Ujerumani katika hatua ya nusu fainali baada ya ndugu Dortmund kushindwa kufuzu mbele ya Madrid.


Huenda kukawa msisimko wa michuano hii kuelekea kwenye fainali ya michuano hii huko Lisbon Ureno baada ya makocha wawili walio wahi kufundisha Chelsea na Madrid kutabiriwa kukutana katika nusu fainali ambao ni Mourinho na Carlo Ancolotti.

No comments:

Post a Comment