Wednesday, 9 April 2014

BA AIPELEKA CHELSEA NUSU FAINALI, MADRID YAPITA JAPO KWA KICHAPO KUTOKA KWA DORTMUND



Siku zote huwa nasema mpira ni mchezo wa dadika 90 na hilo halina ubishi na kwa kusibitisha hilo usiku wa jana tuliweza kushuhudia vijana wa Jose Mourinho wakiibuka na ushindi wa magoli 2 kwa bila dhidi ya Matajiri wa Ufaransa yani Psg.

Magoli hayo mawili ndizo zilikuwa ndoto za special one tangu alipo poteza mchezo wa kwanza kule Ufaransa kwa jumla ya magoli 3 kwa 1 akiwa ugenini, na hivyo kumfanya awe jna kibarua kikubwa zaidi cha kubadili matokeo jambo ambalo alifanikiwa hiyo jana akiwa katika uwanja wa nyumbani.

Goli lililoamsha matumaini ya kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali lilifungwa na Schurrle aliyeingia kuziba pengo la kijana mtundu wa dimba la kati Edun Hazard kunako dk ya 32 na hivyo kuipeleka chelsea mapumziko wakiwa na uhakika wa kusonga mbele.

Mabadiliko ya dakika za lala salama yaliweza kuzika kabisa ndoto za Psg kufika hatua ya nusu fainali na ni pale alipotoka Lampard na kuingia BA kunako dk 66, na ilipofika dakika ya 87 BA aliweza kumkamilishia vizuri kabisa kocha wake safari ya kurudi Bernabeu kwa nusu fainali dhidi ya real madird.

Ba akifunga goli la ushindi
Katika mchezo mwingine uliopigwa huko Ujerumani Real Madrid waliweza kusonga mbele kwa mtaji mzuri wa magoli matatu bila walio shinda nyumbani katika mechi ya kwanza  dhidi ya Dortimund japo ya kukubali kipigo cha goli 2 kwa bila hiyo jana.

Wenyeji wa mchezo huo walioshambulia kwa kasi zaidi katika dakika takribani zote walijipatia goli kunako dk ya 24 kupitia kwa Marco Reus baada ya Real kukosa penati katika dak ya 18 iliyopigwa na Di maria baada ya kipa kuicheza penati hiyo. 

Kunako dk ya 37 tena yule yule Marco Reus aliweka kambani na kufanya mpira uwe wa kasi na ushindani zaidi kwa pande zote mbili huku madrid wakijaribu pia kuliandama lango wa Dortmund mara kwa mara.
Jana Real walishuka dimbani bila ya Ronaldo baada ya kuumia kwenye mechi ya kwanza na hivyo kulipelekea kwa walinzi wa Dortmund kupumzika na kufanya kazi yao kwa kujiamini zaidi kwani safu ya Karimu Benzema na Bale na Di maria haikuwa moto wa kutisha sana.


Reus akishangila na wenzake


Leo ni zamu ya Bayern Munich wakiikaribisha Manchester United huko Alianz Arena baada ya mchezo wa kwnza pale traford kutoka sare ya goli moja kwa moja, huku Atiletico De Madrid wakiwakaribisha  Fc Barcelona baada ya sare ya moja moja pale camp nou katika mechi ya kwanza.

No comments:

Post a Comment