Wednesday, 26 March 2014

BAYERN MUNICH WAPOTEZA LADHA YA BUNDA SLIGA NI BAADA YA KUTANGAZA UBINGWA WAKIWA BADO NA MECHI SABA



Bayern Munich wametangazwa kuwa mabingwa wa ligi kuu ya ujerumani maarufu kama Bungesliga hapo jana baada ya kuwafunga Hertha BSC magoli 3 kwa 1 na kufikisha jumla ya pointi 77 na wakiwa wamecheza michezo 27, na hivyo hakuna timu ya kufikia idadi hiyo ya pointi kwani bado wana michezo saba mkononi.

Borussia Dortmund ndiyo wanashika nafasi ya pili kwa sasa wakiwa na pointi zao 57 na wakiwa wamecheza  michezo 27 sawa na Bayern lakini kukiwa na gepu kubwa la pointi ambalo ni ngumu kulifikia kwa sasa.
 
BEKI WA KATI WA BAYERN AKISHANGILIA NA WENZAKE
Hii inakuwa ni rekodi mpya kwa club hiyo na kwa ligi hiyo pia, lakini imekuwa ni rekodi nyingine kwa kocha wa klabu hiyo Pep Guardiol kuweza kuchukua kombe la ligi huku akiwa na mechi saba mkononi.

Ukiwa ni msimu wake wa kwanza katika klabu ya Bayern tayari ameshaweka kibindoni makombe matatu kati ya matano anayoshiriki na timu yake, ambapo amefanikiwa kuchukuwa Club World Cup, Super Cup, Bundesliga, na sasa bado wamefanikiwa kuingia katika robo fainali ya klabu bigwa ulaya na pia wapo katika hatua ya nusu fainali ya German Cup.

Kwa mana hiyo kama mambo yatakwenda sawa huenda Pep guardiol akaweka rekodi mpya katika vitabu vya ligi hiyo kwa kuwa kocha wa kwanza kuchukuwa makombe yote ambayo ameweza kushiriki kwa msimu moja. 
 
Baada ya mechi ya jana kumalizika pep alisikika akisema kuwa ( Nashukuru tumemaliza salama na tayari tunalo hili kombe mkononi mwetu, lakini napenda kuwashukuru viongozi wa timu na wachezaji pia bila kusahau bechi langu la ufundi pia kwani wao ndo kila kitu. )
Kwa sasakikosi hiko cha  Bayern kimebaki na kazi moja ambayo ni kuhakikisha wanashinda mechi zote saba zilizobaki ili kujiwekea rekodi ya kipekee ya kumaliza ligi huku wakiwa na pointi tisini na moja ( 91 ).

No comments:

Post a Comment