Sunday, 30 March 2014

THE SPECIAL ONE ATANGAZA NJAA KWENYE KIKOSI CHAKE NI BAADA YA KICHAPO KUTOKA KWA CRYSTAL PALACE



Kocha wa vijana wa darajani ( Chelsea ) atangaza njaa kali kwa baadhi ya wachezaji wake na kudai kuwa huenda akafany6a mabadiliko makubwa sana baada ya kupoteza michezo mitatu dhidi ya West Brom, Stoke City, na Crystal Palace.

The special one amedai kuwa baadhi ya wachezaji wameonyesha ubinafsi katika baadhi ya mechi kitendo kilichopelekea Chelsea kupoteza pointi muhimu na kukubali kushuka katika kiti cha kugombania taji la ligi hiyo ya wingereza huku wakibaki na pointi (69).

KOCHA WA CHELSEA JOSE MOURINHO
Mourinho ameenda mbali na kusema bila kuficha kuwa katika mechi  ya juzi na Crystal Palace ambayo walilala kwa bao moja kwa bila, baadhi ya washambuliaji wake walikosa nafasi za wazi kabisa na hivyo kupelekea kupoteza pointi tatu muhimu.

Baada ya mechi hiyo  Mourinho alikaririwa akisema kuwa “ Hili liko wazi na hakuna asiyejua kuwa msimu ujao Chelsea itakuwa na mshambuliaji mpya katika kikosi chake , na kuhusu nini kitatokea kwa wengine basi lipo wazi kama mchezaji atakuwa hana furaha na hajacheza mechi nyingi basi hapa si mahala pake”.

Hadi sasa Chelsea inayo washambuliaji watatu ambao ni Samwel Etoo, Demba Ba, na Fernando Torres, ambao hivi sasa wameshukiwa na zigo la lawama na huenda kukawa na sitofahamu juu ya uwepo wao kunako klabu hiyo ya jiji la London.

Kwa upande huenda klabu ya Chelsea ikafanikiwa kumnyaka mshambuliaji hatari kwa hivi sasa kunako ligi kuu ya spain Diego Costa anayekipiga katika klabu ya Atletico Madrid, na hivyo kupelekea baadhi ya majini kama Torres, David Luiz, Ashey Cole kutokuonekana msimu ujao kweny kikosi hiko.

DIEGO COSTA, KIBOKO YA MAGOLI ANEYEWINDWA NA CHELSEA
Hata hivyo mourinho bado anakibarua kizito zaidi kwenye michuano ya klabu bigwa  ulaya ( UEFA ) dhidi ya matajiri wa ufaransa (PSG) watakapo kutana, na ameahidi kuwa mechi iatkuwa ngumu lakini lazima wapigane kushinda na si vinginevyo.


No comments:

Post a Comment