Monday, 31 March 2014

KRIKETI: UINGEREZA YATUPWA NJE KATIKA TWENTY 20

Timu ya Uingereza ya Kriketi imekamilisha msimu wake kwa njia ya kutanabaisha ikishindwa kufuzu kwa nusu fainali ya kriketi ya twenty 20 baada ya kuambulia kichapo cha mikimbio 45 mikononi mwa timu ya Uholanzi.
WACHEZAJI WA UHOLANZI WAKISHANGILIA USHINDI

 Uingereza ilisajili mikimbio 84 pekee katika ova 11 Uholanzi ilikuwa imeweka jumla ya mikimbio 133-baada ya kuwapoteza wachezaji watano katika ova 20 Katika mechi nyingine iliyochezwa awali, Sri Lanka iliiduwaza New Zealand na mikimbio 59.

Sri Lanka iliweka mikimbio 119 katika Ova 19 huku New Zealand ikimudu mikimbio 60 pekee ilipopoteza wachezaji wake wote.

No comments:

Post a Comment