Monday, 14 April 2014

HUU NDO MWISHO WA ZAMA ZA USIMBA NA UYANGA, KARIBU AZAM WANA WA LAMBA LAMBA



Naweza kuita kama huu ni mwaka wa mapinduzi katika ulimwengu huu wa kwetu wale wapenzia na wafuatiliaji wazuri wa mpira wa miguu duniani kwa ujumla,  kwa kusema kuwa kila kitu kinawezekana kama kweli ukiwa na nia ya  dhati katika jambo husika.

Jana niliweza kushuhudia Stevin Gerrad akijaribu kulia kwa hisia na kuonyesha kuwa ni jinsi gani mpira ulivo sehemu muhimu katika maisha yake na ni baada ya kuwachapa Man city magoli matatu kwa mawili na kuweza kujisogeza karibu kabisa na upepo wa ubingwa wa ligi hiyo ya EPL.

Unajua ni kwanini alilia na kushangilia kwa nguvu? Ni kwasababu bado hajapata nafasi ya kulishika taji la ubingwa wa uingereza tangu aanze kuitumikia klabu hiyo ya liverpool, na sasa anahisi ndo mda wake sahihi wa kuweza kulinyakuwa taji hilo ambalo litakamilisha historia yake baada ya kuweza kunyakuwa mataji mbalimbali ulaya.

Ukiachana na hayo ya huko ulaya turudi hapa kwetu sasa ambapo kila siku tunasema soka letu bado halijakuwa kutokana na mwenendo wa uendeshaji wa ligi yetu na jinsi tulivyo tengeneza ama tunavyo viendesha vilabu vyetu.

Jana kwa mara ya kwanza tuliweza kupata mgeni ama mbabe mpya katika soka la bongo kwa kuchukuwa ubingwa wa ligi kuu bara na kufanikiwa kuvunja ule uyanga na usimba uliyodumu kwa takiribani miaka kumi na nne sasa tangu pale mwaka 2000 alipochukuiwa Mtibwa sukari.

Azam Fc jana waliweza kutangaza ubingwa kwa kuvunja historia ya watoto wa jiji la Mbeya yani Mbeya city kunako uwanja wao wa nyumbani wa sokoine kwa kuwatandika goli mbili kwa moja na kufikisha pointi 59 huku wakiwa na mchezo moja mkononi na hivyo hakuna wa kufikia pointi hizo tena.

Yanga ambao walikuwa wanapewa nafasi ya kunyakuwa taji hilo  wao waliweza kuchomoza na ushindi wa goli mbili kwa moja dhidi ya wenyeji wa mchezo huo ambao ni Jkt Olijoro huko jijini Arusha na kufikisha pointi 55 huku wakiwa na mechi moja mkononi dhidi ya Simba hapo Aprl 19.

washafanya yao
Ni baada ya miaka saba sasa Azam Fc wameweza kukivuna kile ambacho walikipanda mnamo mwaka wa 2008 kwa kupanda daraja na kushiriki rasmi katika ligi kuu ya Tanzania bara maarufu kama ligi kuu ya vodacom.

Kuanzia wachezaji, uongozi wa klabu , mazingira yanayoizunguka klabu kama viwanja vya mazoezi uwanja wao wa nyumbani yani Chamanzi, basi utaweza kukubaliana na mimi kuwa walistahili kuchuwa ubingwa msimu huu au hata iliyopita huko nyuma sema mda ulikuwa bado haujafika nazani.

Nazani tutakuwa tumejifunza kitu kwa sisi wale tulio na uyanga na usimba kuwa kuuza wachezaji nje sio ndo kuendelea kwa mpira wetu bali inatupasa tuwekeze katika mpira kulingana na mapato tunayoingiza kila siku.
Kuchukuwa ubingwa kwa Azam naweza sema kuwa walikubali kuwekeza na walikubali kuvumilia na walikubali kujifunza kutokana na makosa waliofanya misimu ya nyuma na sasa wanaondoka katika jiji la mbeya wakiwa mabingwa wapya wa ligi kuu bara kwa mara ya kwanza.

Kabla ya Azam jana kubeba ubingwa na kuvunja usimba na uyanga vilabu hivi navyo viliweza kuvunja mwiko huu kwa miaka tofauti tofauti, COSMO 1967, MSETO 1975, TUKUYU STARS 1986, COASTAL UNION 1988, MTIBWA SUGAR 1999 NA 2000 NA sasa ni AZAM 2014.

Azam wametupatia darasa la kutosha mashabiki na wadau wa soka hapa Tanzania kwa ujumla kwani hakuna kinachoshindikana kama kweli ukiamua na nazani zikipatikana timu kama Azam ziwe nne basi lazima soka letu linaweza kuifikia nchi kama ya Kenya au Uganda.

Narudia kwa kusema kuwa huu ni mwaka wa maajabu na mapinduzi katika soka na si hapa tanzania tu bali duniani kwa ujumla, baada ya azam sasa nasubiria kuona rafiki yangu Diego Simione akiweza kuchukuwa lile taji la La liga ama kombe la klabu bingwa barani ulaya, hongera Azam kwa hili

No comments:

Post a Comment