Habari njema kwa mashabiki wa klabu ya Manchester united ni
kuwa huenda mshambuliaji wao tegemo kwa sasa katika kikosi hiko Wayne Rooney
akacheza mchezo wa kesho baada ya kuwa nje ya uwanja kutokana na kuumia kidole gumba cha mguu wa kulia kwenye mechi ya
kwanza dhidi ya Bayern wiki iliyopita.
![]() |
| Rooney akiwa mazoezini |
Kocha David Moyes amesibitisha kuwa mshambuliaji huyo
ameshiriki katika mazoezi ya pamoja na wenzake kwa mda wote kabla ya kufunga
safari ya kuelekea Ujerumani kuvaana na mabingwa watetezi wa kombe hilo la uefa
hapo kesho kwenye dimba la Alias Arena.
Kwa upande wa Chelsea wao watafurahia kurejea kwa mpachika
mabao wao aliyekuwa nje kwa kipindi cha wiki mbili Samuel Etoo baada ya kuumia
misuli ya paja na kutoka nje kwenye pambano lao dhidi ya Arsenal huku akifunga
goli la mapema katika ushindi wa goli 6 kwa bila walio upata.
![]() |
| Samwel Eto'o akiwa mazoezini |
Etoo alikosekana kwenye mechi ya kwanza iliyopigwa huko
Paris na kushuhudia Chelsea wakilala kwa goli 3 kwa moja dhidi ya wenyeji PSG, na hivyo kupelekea kwa kocha mwenye
maneno mengi Jose Mourinho kuwa na kibarua kizito leo kwenye dimba lake la
nyumbani pale Darajani.
Hadi sasa Etoo ameweza kushuka dimbani myara 28 msimu huu na
kuweza kufunga magoli 11 katika mechi zote lakini pia ameweza kutoa pasi zilizo
zalisha magoli mara 3 huku akiwa na kadi 1 tu ya njano na hivyo kuwa na rekodi
nzuri baada ya kupewa kipa umbele na kocha wake kama mshambuliaji namba 1.
Naye kocha wa Real Madrid amekanusha tetesi za kuwa huenda
akamtumia winga wake wa gharama duniani Gareth Bale kuziba pengo la mbrazil
Marcelo aliyeumia wiki moja iliyopita watakapo safari kwenye dimba la Iduna
Park kukutana na Borrusia Dortmund kwa mchezo wa marudiano.
![]() |
| Gareth Bale |
Taarifa hizo zilivuma kutokana na mchezaji huyo kuwa
alianzia mpira akicheza kama beki wa kushoto akiwa katika klabu ya Southampton lakini
hata alipo hamia spurs alikuwa akicheza namba hiyo kabla ya kubadilishwa na
kuwa na winga wa kushoto mwenye uwezo wa kucheza kama mshambuliaji.
Bosi huyo wa wafalme hao wa
spain amedai kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kumchezesha beki wa kireno
Fabio Contrao na kumbakiza Bale kunako nafasi yake ile ile na hiyo itasaidia kuongeza zaidi mashambulizi
pale mbele kwa Ronaldo na Karim Benzema.



No comments:
Post a Comment