Wednesday, 2 April 2014

MOYES, GUADIOLA, MARTINO, SIMEONE WOTE WAONDOKA NA POINTI MOJA MOJA KATIKA ROBO FAINALI YA KWANZA YA UEFA

Manchester United yalazimishwa sare ya moja kwa moja katika uwanja wake wa nyumbani maarufu kama MACHINJIONI na mabingwa wapya wa ligi kuu ya ujerumani yani Bayern Munich huku kiungo wa kutumainiwa Bastan Schweinsteiger akisawazisha lakini na kupewa kati nyekundu.
TUMESAWAZISHA

Nemanja Vidic ndiye aliye ifungia United goli la kuongoza  katika dakika ya 58 kupitia mpira wa kona uliopingwa na Wayne Rooney huku Schweinsteiger akisawazisha katika dakika ya 68 baada ya kuunganisha  mpira uliopigwa na Mario Manzukich.

NEMANJA AKIFUNGA GOLI LA KUONGOZA
 Katika mechi nyingine pia Barcelona ililazimishwa sare ya moja kwa moja pia na vinara wa la liga yani Atletico de Madrid katika uwanja wake wa nyumbamni yani Caump new, shukurani za zati ziende kwa Neymar do Santos kwa goli lake la kusawazisha baada ya kuwa nyuma kwa goli moja lililofungwa na Diego Sultan aliye ingia kuchukuwa nafasi ya Diego Costa baada ya kuumia.
DIEGO SULTAN NA WENZAKE WAKISHANGILIA GOLI

Diego Costa alitoliwa nje kunako dakika ya 27 tu ya mchezo huo baada ya kubanwa na nyama za paja na hivyo kumpatia nafasi yake Diego Sultan, amabye aliipatia timu yake goli la kuongoza katika kipindi cha pili cha mchezo huo .

NEYMAR AKISHANGILIA
Katika mchezo wa United Bastan Schweinsteiger alipewa kati nyekundu baada ya kumchezea rafu Wayne Rooney katika dakika za majeruhi na hivyo ataukosa mchezo wa marudiano kunako dimba la Areas Arena huko Ujerumani.

                   
BAADA YA KADI NYEKUNDU

No comments:

Post a Comment