Monday, 31 March 2014

KRIKETI: UINGEREZA YATUPWA NJE KATIKA TWENTY 20

Timu ya Uingereza ya Kriketi imekamilisha msimu wake kwa njia ya kutanabaisha ikishindwa kufuzu kwa nusu fainali ya kriketi ya twenty 20 baada ya kuambulia kichapo cha mikimbio 45 mikononi mwa timu ya Uholanzi.
WACHEZAJI WA UHOLANZI WAKISHANGILIA USHINDI

 Uingereza ilisajili mikimbio 84 pekee katika ova 11 Uholanzi ilikuwa imeweka jumla ya mikimbio 133-baada ya kuwapoteza wachezaji watano katika ova 20 Katika mechi nyingine iliyochezwa awali, Sri Lanka iliiduwaza New Zealand na mikimbio 59.

Sri Lanka iliweka mikimbio 119 katika Ova 19 huku New Zealand ikimudu mikimbio 60 pekee ilipopoteza wachezaji wake wote.

CAFU ATABIRI UBINGWA EPL

Mchezaji gwiji wa Brazil Cafu aipa nafasi Liverpool ya kuchukuwa ubingwa baada ya kuichapa spurs goli nne kwa bila, huku akimnyanyulia mikono kijana kinda wa Liverpool Flanagan kwa kiwango chake bora. Cafu aliyanena ya moyoni kwenye mtandao wake wa twitter na kumpa kinda huyo jina la utani kama REDCAFU, kutokana na kiwango chake kwa sasa na nafasi anayoicheza huku akijifananisha naye.

Sunday, 30 March 2014

THE SPECIAL ONE ATANGAZA NJAA KWENYE KIKOSI CHAKE NI BAADA YA KICHAPO KUTOKA KWA CRYSTAL PALACE



Kocha wa vijana wa darajani ( Chelsea ) atangaza njaa kali kwa baadhi ya wachezaji wake na kudai kuwa huenda akafany6a mabadiliko makubwa sana baada ya kupoteza michezo mitatu dhidi ya West Brom, Stoke City, na Crystal Palace.

The special one amedai kuwa baadhi ya wachezaji wameonyesha ubinafsi katika baadhi ya mechi kitendo kilichopelekea Chelsea kupoteza pointi muhimu na kukubali kushuka katika kiti cha kugombania taji la ligi hiyo ya wingereza huku wakibaki na pointi (69).

KOCHA WA CHELSEA JOSE MOURINHO
Mourinho ameenda mbali na kusema bila kuficha kuwa katika mechi  ya juzi na Crystal Palace ambayo walilala kwa bao moja kwa bila, baadhi ya washambuliaji wake walikosa nafasi za wazi kabisa na hivyo kupelekea kupoteza pointi tatu muhimu.

Baada ya mechi hiyo  Mourinho alikaririwa akisema kuwa “ Hili liko wazi na hakuna asiyejua kuwa msimu ujao Chelsea itakuwa na mshambuliaji mpya katika kikosi chake , na kuhusu nini kitatokea kwa wengine basi lipo wazi kama mchezaji atakuwa hana furaha na hajacheza mechi nyingi basi hapa si mahala pake”.

Hadi sasa Chelsea inayo washambuliaji watatu ambao ni Samwel Etoo, Demba Ba, na Fernando Torres, ambao hivi sasa wameshukiwa na zigo la lawama na huenda kukawa na sitofahamu juu ya uwepo wao kunako klabu hiyo ya jiji la London.

Kwa upande huenda klabu ya Chelsea ikafanikiwa kumnyaka mshambuliaji hatari kwa hivi sasa kunako ligi kuu ya spain Diego Costa anayekipiga katika klabu ya Atletico Madrid, na hivyo kupelekea baadhi ya majini kama Torres, David Luiz, Ashey Cole kutokuonekana msimu ujao kweny kikosi hiko.

DIEGO COSTA, KIBOKO YA MAGOLI ANEYEWINDWA NA CHELSEA
Hata hivyo mourinho bado anakibarua kizito zaidi kwenye michuano ya klabu bigwa  ulaya ( UEFA ) dhidi ya matajiri wa ufaransa (PSG) watakapo kutana, na ameahidi kuwa mechi iatkuwa ngumu lakini lazima wapigane kushinda na si vinginevyo.


Saturday, 29 March 2014

BADO MAPEMA KUMJUA BINGWA NANI KWA SASA KATIKA LIGI YA EPL


Hakika hapa ndipo unapotumika ile kauli ya kusema kuwa asiye fanya kazi na asile, ama kila mbuzi atakula kwa urefu wa kamba yake,  hii nia baadhi ya misemo ambayo hupendwa kutumiwa na wengi pindi panapokuwa na ushindani mkubwa wa kitu flani.
Nimeamua kutumia kauli hizi mbili au misemo hii miwili ambayo ina mana moja nazani katika matumizi ya kila siku.

Huku Pep Guadiola akikamilisha mapema tu kazi ya maafisa wa ligi kuu  ya ujerumani na kuwapa nafasi ya kupanga ratiba ya msimu ujao baada ya kuchukuwa ndoo ya ubingwa mapema tena akiwa na mechi saba mkononi na pia akiweka rekodi ya kipekee zaidi na kikosi cha bayern munich.

Lakini mambo yamekuwa tofauti sana kwa baadhi ya ligi kuu barani ulaya, hususani  kwa ligi kuu ya wingereza maarufu kama ( EPL ), kwani hadi kufikia sasa bado hajajulikana na atakaye tangazwa bigwa  mwishoni mwa msimu huu kati y Chelsea, Man cty, Liverpool, ama Arsenal.

Timu hizi zote bado zina nafasi ya kuchukuwa taji la ligi kama kila mmoja atatumia vizuri makosa atakayo yafanya mwenzake kwa wakati huu uliobakia kwenda kukamilisha mzunguko wa ligi hiyo, lakini ugumu unakuja kutokana na matokeo ambayo yamekuwa yakifanya ligi hii ya  EPL  kutumia ile misemo niliyo anzanayo mwanzo kabisa.

Baadhi ya matokeo ya leo katika ligi hiyo naweza seama yametoa  uhalisia wa jinsi gani ligi hiyo ilivyo na ushindani mkubwa kwani tumeshuudia viojana kutoka darajani (Chelsea ) wakilala goli moja kwa bila dhidi ya Crystal Palace.

Lakin kama hiyo haitoshi baada ya kupata matokeo mazuri katika mechi iliyopita dhidi ya wapinzani wao kutoka jiji moja la Manchester yani man  utd, leo Manchester city  walijikuta wakilazimishwa sare ya goli moja kwa moja dhidi ya vijana wa Arsena Wenger yani Arseanal  ambao wapo nafasi ya nne na pointi zao (64) katika msimamo wa ligi kwa hivi sasa, huku Manchester city wao wakishikilia nafasi ya tatu na pointi zao ( 67 ).

Chelsea yeye anaendelea kubaki na pointi zake zile zile (69) huku akiwa tayari ameshacheza michezo (32), tofauti na yule mabaye anashikilia nafasi ya pili huku akiwa na mchezo pungufu yani (31) na pointi (68) hao si wengine bali ni Liverpool ambao msimu huu naweza sema malengo yao ni kushiriki michuano ya mabingwa barani ulaya yani UEFA baada ya kutokuwepo zaidi ya misimu mitano sasa.

Lakini tukirudi darasani na kuzitumia vizuri kalamu na karatasi kwa msaada wa kikokotoa mahesabu ya calculator ndipo ninapokuja kugungua kuwa  Manuel Pelegrin ni mtu amabye anaweza kulinyakuwa taji hili la EPL kwa mara ya kwanza akiwa na kikosi cha Machester city kwani tayari anazo pointi (67) huku akiwa ameshuka dimbani mara 30 na inakuwa ni tofauti ya michezo miwili na kinara wa ligi hiyo kwa sasa yani Chelsea mwenye pointi (69).

Kwa mahesabu waweza bashiri hivyo lakini kiukweli bado ligi hii inazidi kuchanganya, na ukizingatia bingwa mtetezi nangali bado anasuasua katika nafasi ya saba akiwa na pointi zake (54) huku akiwa tayari na michezo (32).

 Huku nafasi ya juu yake inamilikiwa na Tottenham wakiwa na pointi (56) na michezo (31), na nafasi ya tano inamilikiwa na Everton akiwa na pointi (57) na michezo (30), kwa mana hiyo bado kuna upinzani wa kutosha na chochote kinaweza kutokea na kushuhudia aliye juu akashuka chini, na aliye chini akapanda juu.

Friday, 28 March 2014

JINSI AMBAVYO MOYES ANAUMIZA VICHWA VYA MASHABIKI NA WADAU WA SOKA

     Maoni yangu juu ya Moye's ahondoke au abaki?

kabla sija sema neno lolote naanza na sababu zangu zitakazotowa jibu la swali langu

1. kupoteza ubingwa kw man u na kushika nafasi y 3 kw klabu tajiri duniani hii inaonesh jinsi gani soko la man u linaanza kushuka duniani

2.Msimu ulioisha tarehe 29/3/2013 man u alijikusanyiya points 74 kw mechi 29 na kulikuwa na pengo la point 15 dhidi ya timu iliyo shika nafasi ya pili.Swali la kujiuliza man utd kwa sasa inapoint ngapi na imecheza mechi ngapi na inashika na fasi ya ngapi?

3.man utd msimu huu imepata point ndogo sana kwenye uwanja wake wa nyumbani imezidiwa na Norwich na hull (21 point zilizojipatiya kila mmoja kwenye uwanja wake wa nyumbani).

4.man utd imefunga magoli kwenye uwanja wake wa nyumbani sawa sawa na magoli ya cardif na fulham waliyo ya funga kwenye viwanja vyao vya nyumbani tatizo liko wapi??????

       KUVUNJWA KWA RECORD ZA MAN UTD

1. West brom 2-1 ushindi walio upata pale Old Trafford DEC ndio ulikuwa ushindi wao wa kwanza kuupata OT tokea 1978

2. Everton 1-0 at OT kushinda OT tokea 1992.

3. Yohan Cabaye's goal in DEC at OT, tokea miaka 41 iliyopita newcastle ndio walishinda OT.

4. Tottenham 2-1 at OT tangu miaka 20 iliyopita ndio mara ya mwisho kushinda OT

5. Tokea ianzishwe Swansea ndio mara yao ya kwanza kushinda OT, pale ilipo itoa man u FA Cup.

6. stoke 2-1 tokea mwaka wa 1984 ndio mara ya mwisho kuifunga man utd.

7. 2-0 against olimpiakos ndio mara ya kwnza man u kufungwa na timu kutokea ugiriki.

michezo na mashabiki
KOCHA WA MAN UTD, DAVID MOYES

                       Hii ni kutoka kwa mdau mmoja wa ligi ya wingereza..
                SWALI JE MOYE'SAENDELEE KUPEWA NAFASI??????

Wednesday, 26 March 2014

BAYERN MUNICH WAPOTEZA LADHA YA BUNDA SLIGA NI BAADA YA KUTANGAZA UBINGWA WAKIWA BADO NA MECHI SABA



Bayern Munich wametangazwa kuwa mabingwa wa ligi kuu ya ujerumani maarufu kama Bungesliga hapo jana baada ya kuwafunga Hertha BSC magoli 3 kwa 1 na kufikisha jumla ya pointi 77 na wakiwa wamecheza michezo 27, na hivyo hakuna timu ya kufikia idadi hiyo ya pointi kwani bado wana michezo saba mkononi.

Borussia Dortmund ndiyo wanashika nafasi ya pili kwa sasa wakiwa na pointi zao 57 na wakiwa wamecheza  michezo 27 sawa na Bayern lakini kukiwa na gepu kubwa la pointi ambalo ni ngumu kulifikia kwa sasa.
 
BEKI WA KATI WA BAYERN AKISHANGILIA NA WENZAKE
Hii inakuwa ni rekodi mpya kwa club hiyo na kwa ligi hiyo pia, lakini imekuwa ni rekodi nyingine kwa kocha wa klabu hiyo Pep Guardiol kuweza kuchukua kombe la ligi huku akiwa na mechi saba mkononi.

Ukiwa ni msimu wake wa kwanza katika klabu ya Bayern tayari ameshaweka kibindoni makombe matatu kati ya matano anayoshiriki na timu yake, ambapo amefanikiwa kuchukuwa Club World Cup, Super Cup, Bundesliga, na sasa bado wamefanikiwa kuingia katika robo fainali ya klabu bigwa ulaya na pia wapo katika hatua ya nusu fainali ya German Cup.

Kwa mana hiyo kama mambo yatakwenda sawa huenda Pep guardiol akaweka rekodi mpya katika vitabu vya ligi hiyo kwa kuwa kocha wa kwanza kuchukuwa makombe yote ambayo ameweza kushiriki kwa msimu moja. 
 
Baada ya mechi ya jana kumalizika pep alisikika akisema kuwa ( Nashukuru tumemaliza salama na tayari tunalo hili kombe mkononi mwetu, lakini napenda kuwashukuru viongozi wa timu na wachezaji pia bila kusahau bechi langu la ufundi pia kwani wao ndo kila kitu. )
Kwa sasakikosi hiko cha  Bayern kimebaki na kazi moja ambayo ni kuhakikisha wanashinda mechi zote saba zilizobaki ili kujiwekea rekodi ya kipekee ya kumaliza ligi huku wakiwa na pointi tisini na moja ( 91 ).