Monday, 15 February 2016

TERRY KUIKOSA PSG KATIKA GAME YA KESHO YA UCL

Jinamizi la majeruhi limeendelea kuwandama mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Chelsea, baada ya safari hii wodi yao kumpokea captain John Terry.

Terry aliumia kwenye mchezo wake wa 699 akiwa na jezi ya Chelsea dhidi ya Newcastle United, huku wakiibuka na ushindi wa magoli 5-0.

Taarifa za ndani zinasema kuwa Terry ameshindwa kusafiri na timu jioni ya leo kwenda ufaransa katika pambano la michuano ya uefa champion league hatua ya mtoano dhidi ya PSG.

Lakini pia taarifa nzuri ni kuwa mchezaji aliye katika kiwango cha juu kwa sasa Oscar amerejea kikosi na kufanikiwa kusafiri na timu ..

Kwa upande mwingne Terry atalazimaka kusubiri kupona ili kukamilisha mchezo wake wa 700 akiwa na kikosi chake hiko kabla ya kuachana na miamba hyo ya London  mwishoni mwa msimu huu
Source :skysports

KUNA EL CLASICO INAKUJA KATIKA MANCHESTER DEBY

Ni vita inayosubiriwa kwa hamu kubwa san. Ni vita inayosubir masaa tu kutimia km sio siku mwezi au miezi. Yan ni vijana wawili ambao wakati wa ujana waliishi katika kijiji kimoja pale catalunya katika nchi ya spain wakiwa katik club ya Barcelona. Huku mmoja akiwa km mchezaji wa club hyo na mwingne akiwa km  kocha msaidizi wa club hyo. Weng wetu tunafahamu hii story ya watu hawa wawili
Lakini sasa kuna story mpya inakuja ambayo  wengi wetu tunasubiri kuiskia na kushuhudia pia .
Wiki chache zilizopita club tajiri ya ligi kuu nchini English Manchester city kupitia kocha wake manual pelegrin aliweka wazi kuwa mwisho wa msimu ataachia kibarua chake na kumkabidhi pep guadiol kama kocha mpya wa timu hiyo.
Manual alienda mbali zaidi na kusema kuwa alifahmu hilo tangu awali na hata kwenye mkataba wake mambo yapo wazi kabsa.

Kwa upande wa pili wa majirani zao mambo yamezidi kuwa sio mambo na kuna taarifa zimezagaa katika vyombo mbalimbali vya habar dunian kuwa huenda kocha wa sasa mdachi huyu loui van gaal asimalize mwaka wake wa mwisho katika  mkataba wa  miaka  mitatu  na mashetani hao wa Manchester United baada ya mfululizo wa matokeo yasiyo ridhisha kwa mashabiki mbalimbali wa timu hyo pamoja na wadhamini wao wakuu adidas.
Na sasa huenda kocha wa zaman wa Chelsea aliyetimuliwa kazi mwezi moja nyuma katika jiji la London jose mourihno akachukuwa nafasi ya mdachi huyo.
Taarifa za ndani zinasema kuwa tayari mabosi wa United washakubaliana na mreno huyo kwa mkataba wa miaka mitatu kwa kuinoa club hiyo ambayo haifanikiwa kuchukuwa taji lolote tangu kuandoka kwa sir Alex Ferguson.
Kama mreno huyu atafanikiwa kupewa timu hii basi itakuwa ni mkomoano wa majirani hawa wa mji mmoja yani  Manchester United na Manchester city kwa kuwatumia hawa vijana ambao wamejizolea umaarufu na sifa kubwa kwa ufundishaji w soka lao katika club mbalimbali walizo pitia ... tusubir  kuona el clasico nyingine ya mreno na mspain pale katika Manchester deby.
Karibu sana England bwana pep

Tuesday, 22 April 2014

BREAKING NEWS; DAVID MOYES AFUKUZWA RASMI MAN UTD

Kwa taarifa zilizotoka hivi punde ni kuwa aliyekuwa kocha Man Utd amefukuzwa rasmi kunako klabu hiyo
Moyes aliyudumu kwa miezi kumi katika kiti hiko cha ukocha katika klabu hiyo amefukuzwa baada ya kuwa na mfululizo wa matokeo duni akiwa kama mwalimu wa klabu hiyo.
David Moyes

Moyes ameweza kupoteza mechi sita katika uwanja wa nyumbani msimu huu, huku akiipeleka klabu hiyo nje ya michuano ya klabu bigwa barani ulaya yani UEFA ambapo kwa mara ya mwisho Utd kutoshiriki ilikuwa mwaka 1995.


Monday, 21 April 2014

BREAKING NEWS- MOYES KUONDOKA OLD TRAFFORD






Kwa habari zilizozagaa kwenye mitandao muda huu,kuna habari inayoelezea kuwa kocha wa Man utd David Moyes huenda akaondoka Old trafford

Bodi ya timu ya manchester wameshindwa kuvumilia suala hili baada ya kipigo cha jana cha 2-0 dhidi ya timu Everton.

Magazeti  kama Daily telegraph,daily mail na the guardian yote yameripoti kuhusu habari hii leo hii hivyo huenda Moyes asiweze kumalizia mechi nne zilizobakia.

klabu ya Manchester united mpaka sasa imeshindwa kukanusha juu ya habari hii,na viongozi walipoulizwa walijibu suala la kumfukuza Moyes ni suala suala linaloweza kutolea muda mchache ujao.

mwandishi-ALLY GININGI SHAMBI

Wednesday, 16 April 2014

EVERTON YAPUNGUZWA KASI, HUKU MAN CTY YALAZIMISHWA SARE YA KIPORO CHAKE DHIDI YA SUNDERLAND

mashabiki wa everton waliungana na wenzao wa liverpool kuwakumbuka mashabiki waliopoteza maisha katika  FC Hillsborough disaster kabla ya mchezo.
 Klabu ya Everton leo imepunguzwa kasi ya kuweza kuwania nafasi ya nne kwajili ya kushiriki ligi ya mabigwa barani ulaya UEFA baada ya kupokea kichapo kutoka kwa Crystal Palace na hivyo kurudi nafas ya 5.

 Nao Man cty wamelazimishwa sare na sunderland walio kweny nafasi ya mwisho ya msimamo wa ligi, baada ya kucheza mechi amabayo ilikuwa ni kiporo kwa timu zote mbili, na sasa Man cty anabaki na alama 71 huku bado akiwa na mchezo mkononi.

wickham akifunga goli la kwanza

KLABU MOJA WAPO KATI YA HIZI NNE LAZIMA ITAANDIKA REKODI MPYA KAMA IKIWA BINGWA WA UEFA



Mambo ambayo yanaweza kutokea na kuwa historia mpya na ya kipekee katika soka hususani katika ligi ya mabingwa barani ulaya yani UEFA, kwa msimu huu ambao tumeweza kushuhudia vilabu mbalimbali vikitoa upinzani wwa kutosha kwa vilabu kongwe katika ligi hiyo.

Tukianza na klabu ya Atletico de Madrid akiongozwa na Diego Simione ameweza kutoa upinzani mkubwa sana msimu huu akianzia katika ligi kuu ya spain yani La Liga na hadi sasa inaongoza ligi hiyo kwa tofauti ya pointi nne dhidi ya Barcelona.

Atletico imeingia katika hatua ya nusu fainali kwa kuwasambaratisha vizuri tu vigogo wengine kutoka katika ligi moja nao ambao ni fc Barcelona kwa jumla ya magoli 2 kwa 1 na hivyo kupelekea wao kuweza kuingia katika hatua hiyo ya nusu fainali na kukutana na Chelsea.

Kama watafanikikupita  kupita katika hatua hii na kuingia fainali na kufanikiwa kuchukua kombe hili namba mbili kwa umarufu duniani basi watakuwa wameweka rekodi mpya katika klabu tangia kuanzishwa yapata miaka 40 sasa kuchukuwa kombe hilo la UEFA kwa mara ya kwanza, Hiyo itakuwa ni kwa upande wa wababe hawa wapya wa ligi ya spain.

Kwa upande wa mabingwa wapya na wa kihistoria wa Ujerumani Bayern wao wameweza kuingia kwenye hatua ya nusu fainali baada ya kuwachabanga vilivyo mashetani wekundu wa jiji la manchester kwa jumla ya magoli 4 kwa 2 na kukata tiketi hiyo na sasa watkutana na Real Madrid.

Klabu hii inayongozwa  na kocha aliyejizolea makombea mbalimbali akiwa na Fc Barcelona Pep Guadiola kama itaweza kuchukuwa kombe hili basi itakuwa ni timu ya kwanza katika historia ya michuano hii kubeba kombe hili mara mbili mfululizo kwani wao ndo mabingwa watetezi hadi hivi sasa.

Kwa upande wa klabu ya Chelsea inayonolewa  na kocha mreno mwenye maneno mengi kama wasemavyo mashabiki wa soka dunia kwa ujumla Jose Mourinho, kama itafanikiwa kuchukua kombe hili basi itakuwa ni historia mpya kwa kocha huyo kuchukuwa kombe hili mra tatu akiwa na timu tatu tofauti na katika nchi tatu tofauti duniani.

Nao Real Madrid ambayo imeweza kuchukuwa kombe hili kwa mara 9 na kuwa klabu inayo ongoza katika hisoria ya michuano hii, basi kama itaweza kubeba tena kombe hili itakuwa ndiyo klabu ya kwanza katika historia kuweza kufikia nambari 10 au ( double digit number )

Je ni nani ataweza kuibuka mshindi na kuweka historia mpya katika klabu yake kati yao?, hili ni swali ambalo nazani tunaweza kulijibu kunako usiku wa tarehe 22 mwezi huu kati nchi ya Spain ambapo ndipo mechi zote za hatua ya nusu fainali zitaanzia.




GARETH BALE ASIBITISHA KUWA YEYE NIA HATARI BAADA YA KUIPATIA REAL UBINGWA WA 19 WA COPA DEL REY



Real Madrid katika picha ya ubingwa


Real  Madrid wameweza kuibuka na ushindi wa magoli  mawili kwa kwa moja dhidi ya mahasimu wao wakubwa Barcelona katika mchezo wa fainali wa kombe la Copa del rey.

Real wao ndio walikuwa wa kwanza kupachika goli kunako dk ya 11 kupitia kwa Angel Di maria,  na hivyo kufanya hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Real walitoka wakiwa kifua mbele katika awamu hiyo.

Kunako kipindi cha pili  katika dk ya 68 kinda wa Barcelona  Marco  Bartra aliweza kusawazisha bao hilo kupitia mpira wa kichwa baada ya kuitumia vizuri kona iliyo chongwa na nahoza wake Xavi.

Baada ya goli hilo Barcelona waliweza kuamka na kujaribu kuonyesha mpira ulio takata  kama ilivyo kawaida yao, lakini kunako dakika za lala salama Gareth Bale aliweza kuifungia real goli la ushindi.
di maria akishanglia goli la kwanza

Bale aliweza kusibitisha kuwa yeye ni mchezaji ghali zaidi duniani baada ya kumshinda mbio kinda Marco Bartra na kwenda kumuona golikipa Pito kunako dk ya 85 ya mchezo huo.

bale akishangilia goli la ushindi
Mchezo huo ambao ulitawaliwa na kadi 5 za njano pia ulikuwa ni mchezo usio isha tamwe za hapa na pale baina ya wachezaji wa timu hizi mbili, huku real wakiwa wameshuka dimbani bila ya Cristian Ronaldo baada ya kupata majeraha ya nyama za pacha katika mechi iliyopita.

Hii inakuwa ni kwa mara ya 19 kwa real madrid walio chini ya Carlo Ancelotti kuweza kuchukuwa kombe hili la Copa Del Rey  tangu lianzishwe na mara ya mwisho walichukuwa mwa 2010-2011 na mara ya kwanza ilikuwa ni 1905.

hakuna kama mimi
Hili linakuwa ni kombe la kwnza kwa Real Madrid kuweza kuchukuwa katika msimu huu, huku wakiwa bado katika kugombania ubingwa wa ligi dhidi ya vinara wa ligi hiyo kwa sasa ambao ni Atiletico De Madrid wenye alma 82 kwa 79 za real.

Lakini pia unakuwa ni ubingwa wa kwanza kwa Carlo Ancelotti akiwa na klabu hiyo huku bado akiwa na kibarua kizito cha kuipatia Real ubingwa wa mara ya 10 wa klabu bingwa barani ulaya baada ya kuingia hatua ya nusu fainali na watakipiga na Bayern Munich ya Ujerumani tarehe 22 mwezi huu.