Monday, 15 February 2016

TERRY KUIKOSA PSG KATIKA GAME YA KESHO YA UCL

Jinamizi la majeruhi limeendelea kuwandama mabingwa watetezi wa ligi kuu ya England Chelsea, baada ya safari hii wodi yao kumpokea captain John Terry.

Terry aliumia kwenye mchezo wake wa 699 akiwa na jezi ya Chelsea dhidi ya Newcastle United, huku wakiibuka na ushindi wa magoli 5-0.

Taarifa za ndani zinasema kuwa Terry ameshindwa kusafiri na timu jioni ya leo kwenda ufaransa katika pambano la michuano ya uefa champion league hatua ya mtoano dhidi ya PSG.

Lakini pia taarifa nzuri ni kuwa mchezaji aliye katika kiwango cha juu kwa sasa Oscar amerejea kikosi na kufanikiwa kusafiri na timu ..

Kwa upande mwingne Terry atalazimaka kusubiri kupona ili kukamilisha mchezo wake wa 700 akiwa na kikosi chake hiko kabla ya kuachana na miamba hyo ya London  mwishoni mwa msimu huu
Source :skysports

KUNA EL CLASICO INAKUJA KATIKA MANCHESTER DEBY

Ni vita inayosubiriwa kwa hamu kubwa san. Ni vita inayosubir masaa tu kutimia km sio siku mwezi au miezi. Yan ni vijana wawili ambao wakati wa ujana waliishi katika kijiji kimoja pale catalunya katika nchi ya spain wakiwa katik club ya Barcelona. Huku mmoja akiwa km mchezaji wa club hyo na mwingne akiwa km  kocha msaidizi wa club hyo. Weng wetu tunafahamu hii story ya watu hawa wawili
Lakini sasa kuna story mpya inakuja ambayo  wengi wetu tunasubiri kuiskia na kushuhudia pia .
Wiki chache zilizopita club tajiri ya ligi kuu nchini English Manchester city kupitia kocha wake manual pelegrin aliweka wazi kuwa mwisho wa msimu ataachia kibarua chake na kumkabidhi pep guadiol kama kocha mpya wa timu hiyo.
Manual alienda mbali zaidi na kusema kuwa alifahmu hilo tangu awali na hata kwenye mkataba wake mambo yapo wazi kabsa.

Kwa upande wa pili wa majirani zao mambo yamezidi kuwa sio mambo na kuna taarifa zimezagaa katika vyombo mbalimbali vya habar dunian kuwa huenda kocha wa sasa mdachi huyu loui van gaal asimalize mwaka wake wa mwisho katika  mkataba wa  miaka  mitatu  na mashetani hao wa Manchester United baada ya mfululizo wa matokeo yasiyo ridhisha kwa mashabiki mbalimbali wa timu hyo pamoja na wadhamini wao wakuu adidas.
Na sasa huenda kocha wa zaman wa Chelsea aliyetimuliwa kazi mwezi moja nyuma katika jiji la London jose mourihno akachukuwa nafasi ya mdachi huyo.
Taarifa za ndani zinasema kuwa tayari mabosi wa United washakubaliana na mreno huyo kwa mkataba wa miaka mitatu kwa kuinoa club hiyo ambayo haifanikiwa kuchukuwa taji lolote tangu kuandoka kwa sir Alex Ferguson.
Kama mreno huyu atafanikiwa kupewa timu hii basi itakuwa ni mkomoano wa majirani hawa wa mji mmoja yani  Manchester United na Manchester city kwa kuwatumia hawa vijana ambao wamejizolea umaarufu na sifa kubwa kwa ufundishaji w soka lao katika club mbalimbali walizo pitia ... tusubir  kuona el clasico nyingine ya mreno na mspain pale katika Manchester deby.
Karibu sana England bwana pep